UPENDO WA KWELI
UPENDO WA KWELI
Katika maisha yangu
ya imani na miito, ni vyema kujikumbusha na kuelewa kwamba ‘Mungu ananijua
zaidi ya ninavyo jijua mimi’ na pia “Mungu ananipenda zaidi ya ninavyo jipenda
mimi”. Ananijua na ananipenda, kwahiyo ni jukumu na wajibu wangu mimi kama
kijana kuwa mtu wa KUMWAMINI.
Kuna
mambo makuu matatu ambayo ni ya msingi
saaana mimi kama kijana yanipasa kuyashiriki na kuyaishi. Kuyatambua mambo haya
tujiiulize maswali kwa uaminifu;
Moja, je, nipo katika hali ya neema?- Kuishi maisha ya neema ni kule kuwa
katika namna ambayo ni ya kumpendeza Mungu; Hali ya kuishi maisha ya usafi wa
moyo, kuyapenda masakramenti ya kanisa, kujitoa kwa ajili ya wale wasiojiweza
hasa masikini , wagonjwa na wote walio katika mazingira magumu, kulipenda na
kuliishi neno la Mungu, kuishi maisha yasio ya pande mbili, kuyapenda mambo ya
kiroho na pia kuwa katika hali ambayo sio ya dhambi. Hii ndio hali ya neema
hali ambayo yampasa kijana kijana yeyote aiishi, mimi nitajivunia na kutambua
kwamba naiishi hali ya neema pale ninapoishi maisha ya kumpenda Mungu na jirani
yangu. Swali la pili kujiuliza ni kwamba
Je, natimiza wajibu wangu wa kila siku?,
kulingana na rika letu na shughuli zangu za kila siku , ikiwa mimi ni
mawanafunzi ninalazimika kusoma kwa bidii na kutumia vyema mda wangu ili niweze
kufanikiwa katika masomo yangu. Cha kwanza kwanza,wajibu wangu wa kwanza kama
mwanafunzi ni kusoma kwahiyo nilazima mimi kuyatanguliza masomo yangu mbele ya
vyote, kama nimfanyakazi lazima kuithamini kazi yangu na kuipenda. Sisi kama
vijana ni tunakumbushwa kwamba ni wajibu wetu kuyatunza mazingira, kusaidia
wanafamilia, kuwasahihisha wanaoenda kinyume cha maadili, kutenda yaliyo mema
siku zote. Mimi kama kijana ni wajibu wangu kuutumia vyema uhuru
niliojaliwa na
mwenyezi Mungu kwa kuisha kwa maadili na kwa kumcha Mungu, niitumie vyema
teknologia, simu yangu isiniongoze bali niiongoze mimi, nitambue mimi kama
kijana kila kitu kina muda wake katika maisha na pia kukataa kudanganyika.
Swali la tatu mimi kama kijana linalonipasa kujiuliza ni je, nilisali
leo? Kati ya mambo ya msingi ambayo kijana mcha Mungu hanabudi kuyafuata ni
kuwa mtu wa sala. Mtu wa sana ni yule siku zote hutafakari na huwa na fikra
zilizo njema anayetambua mapungufu yake na kumrudia Mungu, anayependa na
kulifuata neno la Mungu, anaye shiriki masakramenti ya kanisa na anayezungumza
na Mungu na kumkabithi maisha yake ayatawale. Sala ni silaha ya pekee thidi ya
muovu shetani, kujana anayependa maisha ya sala huwa na moyo wa kutafakari juu
ya maisha yake na kufanya chaguzi zilizo jema juu ya maisha yake.
Mimi kama
nisipokuwa katika hali ya Neema, nisipo fanya yale ninayopaswa kufanya, nisipo
timiza wajibu wangu wa kila siku ni sawa na kusema Hapana kwa Mungu. Mimi kama
kijana nijiwekee ratiba yangu ambayo nahitaji kuifuata, ni kipi nikifanye ili
niweze kuwa katika hali ya neema, kama sisali yanipasa nianze kusali, muda
wangu ninaoupoteza kwenye mitandao ya kijamii kutuma na kupekua maambo yasiyo
faa, yaniapasa kuacha. Pambano bila upinzani halifurahishi tujiwekee mipaka
katika maisha yetu ili tuweze kuyafurahia maisha yenye fanaka mbeleni. Wakusoma
wasome kwa bidii zote na wakufanya kazi wafanye kwa uaminifu na kwa nguvu zao
ili waweze kuvuna kadiri wapandavyo. Tukumbuke Mungu akiwa katikati ya shughuli
zangu hakika hakuna kitakachoshindikana. Ni wajibu wangu kusema kweli ndani ya
moyo wangu, kama ninaumwa sikio langu ni lazima nimwambie dactari ukweli kuhusu
sikio langu ili niweze kupata matibabu mazuri. Tusijidanganye tuseme kweli na
tutasimama imara katika hii safari ya kutambua miito yete.
Comments
Post a Comment